JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

PAC YAIAGIZA TBA KUKAMILISHA JENGO LA MAADILI KWA WAKATI.
13 Mar, 2024
PAC YAIAGIZA TBA KUKAMILISHA JENGO LA MAADILI KWA WAKATI.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) imeagiza Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) kukamilisha mradi wa ujenzi wa jengo la Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa wakati.

Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Naghenjwa Kaboyoka alitoa agizo hilo wakati wa ziara ya wajumbe hao  waliyofanya katika mradi wa jengo la Sekreterieti ya Maadili linalojengwa katika mtaa wa Kilimani jijini Dodoma. Ziara hiyo ilifanyika tarehe 13  Machi, 2024.

”Mradi huu umekua na nyongeza ya mkataba kwa muda wa miezi 17  jambo ambalo linaweza likaipa Serikali yetu hasara kwa hiyo niwaombe wenzetu wa TBA mkamilishe mradi huu kwa wakati kulingana na mkataba wa sasa unavyotaka,” alisema.

Kwa mujibu wa mkataba wa awali, jengo hilo lilitakiwa kukamilika Desemba 15, 2022 ambao umeongezwa hadi tarehe 3 Mei, 2024.

Wajumbe wa kamati wameeleza kuwa kutokamilika kwa wakati kwa mradi huo kunaisababishia hasara serikali kwa kuendelea kulipia Sekretarieti ya Maadili gharama za pango ambazo zingetumika kufanya shughuli nyingine za maendeleo.

Katika hatua nyingine, Bw. John Kaole, Katibu Usimamizi wa Maadili, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ameiambia Kamati ya Bunge kuwa ujenzi wa jengo hilo utagharimu kiasi cha shilingi 9,064,275,060.04.

Alieleza kuwa ujenzi huo, ulianza 14 Juni,2019 na mpaka sasa umefikia asilimia 95%.

Ziara hiyo ilijumuisha wajumbe wa Kamati ya Bunge, wajumbe kutoka Sekretarieti ya Maadili, Wajumbe kutoka Wakala wa majengo Tanzania pamoja na  wajumbe kutoka Ofisi ya  Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >