JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Orodha ya makosa ya  ukiukwaji wa maadili kuhuishwa
30 Nov, 2023
Orodha ya makosa ya  ukiukwaji wa maadili kuhuishwa

Orodha ya makosa ya  ukiukwaji wa maadili kuhuishwa

Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma imeanza mchakato wa kufanya marekebisho ya makosa ya ukiukwaji wa maadili kwa mujibu wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma Namba 13 ya mwaka 1995, kwa lengo la kuboresha kifungu cha 19 (1) cha sharia hiyo  chenye orodha ya  makosa ya ukiukwaji wa maadili kwa Viongozi wanaowajibika na Sheria ya Maadili ya Viongozi wa umma.

Akifungua kikao kazi hicho Katibu Idara ya Ukuzaji Maadili, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Bw. Waziri Kipacha, alisema kuwa, Sekretarieti ya Maadili imechukua uamuzi huo wa kupitia upya na kuhuisha viambata vya makosa hayo ya ukiukwaji wa maadili, kutokana na mabadiliko ya Sheria ya Maadili pamoja na Kanuni zake ambayo imeongeza wigo wa makosa ya sheria.

“Tukae tujadili makosa haya, na kama kwa mujibu wa mabadiliko ya Sheria yaliyofanyika tukaona kuna haja ya kuongeza makosa yaliyoongezwa kupitia Kanuni mbalimbali zilizofanyiwa marekebisho tuongeze, lakini pia, kama tutaona kuna haja ya kuboresha, tuboreshe, ili Taasisi yetu iweze kusimamia  haki kwa Viongozi tunaowasimamia” alisema.

Kwa mujibu wa Bw. Kipacha alieleza kuwa, Sheria ya Maadili imeeleza kuwa, uchunguzi unaotakiwa kufanywa na Sekretarieti ya Maadili ni Uchunguzi wa awali utakaopelekwa katika  Baraza la maadili kwa ajili ya  kufanya Uchunguzi wa kina hivyo ni wajibu wa Taasisi kufanya uchunguzi huo kwa umakini wa hali ya juu na kujiridhisha wazi ni kosa gani la kimaadili  ambalo kiongozi husika amekiuka.

“Taasisi hii, inawachunguza Viongozi wenye hadhi kubwa, kwa hiyo ni dhahiri kuwa, tunapaswa kutekeleza kazi hiyo ya uchunguzi kwa uadilifu na uweledi mkubwa, ili kulinda heshima na hadhi za viongozi hao” alisema.

Aidha, Bw. Kipacha, alisisitiza umuhimu wa kikao kazi hicho kuwa, kina kazi ya  kuhakikisha kwamba  kinatoa mapendekezo yatakayoiwezesha Taasisi kutekeleza majukumu yake vizuri ya kuisimamia Sheria.

“Naamini kuwa, baada ya kikao kazi hiki, tutatoka na viambata vya makosa ya ukiukwaji wa Maadili ambavyo vitatusaidia katika kukamilisha na kupata ushahidi wa kutosha ili tuweze kupeleka mashauri yetu katika Baraza la Maadili, ambalo ndilo lenye mamlaka ya kutoa mapendekezo kwa mamlaka ya nidhamu ya Kiongozi husika kwa ajili ya kuchukuliwa hatua za kinidhamu”, alisema.

 

Awali, akimkaribisha mgeni rasmi, Mkuu wa Kitengo cha huduma za Sheria, Bi. Emma Gelani, alieleza kuwa, kikao kazi hicho cha siku tatu kitafanya kazi ya kipitia upya na kuhuisha viambata vya  makosa ya ukiukwaji wa Sheria ya Maadili, kwa lengo la kusaidia na kuwezesha kazi ya kiuchunguzi kuwa rahisi katika utekelezaji wa kazi zao, kama za kukusanya ushahidi utakaopelekea kuwa na matokeo mazuri mbele ya Baraza la Maadili.

Makosa ya ukiukwaji wa Maadili yameainishwa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yam waka 1977, Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma pamoja na  Kanuni zake.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >