JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

MWANGESI: WAHARIRI TUMIENI KALAMU ZENU KUANDIKA UMHIMU WA MAADILI KWA VIONGOZI
25 May, 2024
MWANGESI: WAHARIRI TUMIENI KALAMU ZENU KUANDIKA UMHIMU WA MAADILI KWA VIONGOZI

Wahariri wa Vyombo vya Habari nchini wametakiwa kutumia kalamu zao kuandika umuhimu wa maadili kwa viongozi wa umma ili kusaidia kukuza uadilifu wao katika utendaji wa kuwatumikia Wananchi na kuleta maendeleo.

Wito huo, umetolewa na Kamishna wa Maadili Mheshimiwa Jaji (Mst.) Sivangilwa Mwangesi wakati akifungua mkutano wa Jukwaa la Wahariri wa vyombo vya Habari nchini uliolenga kuwajengea uelewa kuhusu Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma Na 13 ya mwaka 1995 pamoja na mafanikio ya miaka mitano. uliofanyika Leo Mei,24, 2024 katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania mkoani Dar es Salaam.

“Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma peke yake haiwezi kutoa elimu ya uadilifu bila msaada wa wadau wengine mkiwemo nyie wahariri wa vyombo vya Habari tunawategemea sana” alisema Jaji Mwangesi.

Mhe. Jaji (Mst) Mwangesi aliwasisitiza Wahariri Kwenda kuandika makala za kichambuzi, kufanya mahojiano na wataalamu wa masuala ya maadili pamoja na wananchi, kufanya uchunguzi wa kina na kuandika ripoti za kuchambua tabia na maadili ya Viongozi kwa kina.

Aidha, Kamishna Mwangesi amelipongeza Jukwaa la Wahariri kwa ushirikiano wanaoutoa kila siku kwa Sekretarieti ya Maadili kwa kuendelea kuchapisha habari zinazohusu uadilifu wa viongozi wa umma nchini.

Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, Bw. Sadick Yassin ameiomba Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuongeza nguvu ya kutoa elimu kwa wananchi ili waijue vizuri ofisi pamoja na majukumu yake na kuongeza wigo wa kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi.

“Ikiwezekana mutumie mitandao ya kijamii, kubandika ata matangazo kwenye nguzo na mbao mbalimbali ili wananchi waijue vizuri ofisi”alisema

Akielezea mafanikio ya Sekretarieti, Mkurugenzi wa ufuatiliaji na mipango Bw. Omary Juma alisema kwa kipindi cha miaka 2 iliyopita wastani wa uwasilishaji malalamiko kwa mwezi umeongezeka kutoka malalamiko 16 mwaka 2021/22 hadi malalamiko 18 kwa mwaka 2022/23.

"Ongezeko hilo ni sawa na 13% hali hii inaonyesha vyombo vya Habari nchini vimekuwa na mchango mkubwa wa kutoa elimu na kupelekea wananchi kupata uelewa juu ukiukwaji wa maadili.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >