JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Mwangesi: Maadili yanapaswa kuanza na sisi wenyewe.
27 Oct, 2023
Mwangesi: Maadili yanapaswa kuanza na sisi wenyewe.

Watumishi wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Kanda ya Nyanda za Juu Kusini – Mbeya wametakiwa kuzingatia maadili wao wenyewe kabla ya kuwahimiza wengine kufanya hivyo.

Wito huo umetolewa na Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji Sivangilwa Mwangesi wakati akizungumza na Watumishi hao jijini Mbeya alipofanya ziara ya siku mbili mkoani Mbeya ikiwa ni mara yake ya kwanza kutembelea Ofisi hizo tangu ateuliwe kushika wadhifa huo mwezi Desemba, 2020.

“Tuna wajibu mkubwa wa kuitetea taasisi yetu kwa kuzingatia viwango vya juu vya maadili wakati tunapotekeleza majukumu yetu kabla ya kuwahimiza wengine kufanya hivyo.Itakuwa ni aibu ikiwa wewe msimamizi wa maadili ukikiuka maadili.Nawasihi kufanya vile jamii na Serikali inavyotarajia tuyafanye”alifafanua Mhe. Mwangesi.

Kuhusu utunzaji wa siri, Mhe. Mwangesi alisema kuwa taasisi hii inatunza taarifa nyeti za viongozi wa umma hivyo hategemei kuona taarifa hizo zinazagaa mitaani na kuwasihi watumishi hao kujisahihisha kwa yale ambayo wanahisi kuwa hayapo sawa.

Akijibu changamoto iliyowasilishwa na Katibu Msaidizi wa Kanda hiyo Bw. Paul Kanoni kuhusu ufinyu wa bajeti unaokwamisha utekelezwaji wa mpango kazi wao, Mhe. Mwangesi alisema kuwa changamoto hiyo ni ya kitaifa na kwamba inatokana na Serikali kuelekeza fedha nyingi katika ukamilishwaji wa miradi mikubwa ya taifa ya maendeleo na kuwaasa kuendelea kutumia vizuri fedha inayopatikana huku wao kama viongozi wa taasisi wakiendelea kuziomba mamlaka husika kuiongezea taasisi hiyo ukomo wa bajeti yake.

Awali, Mhe. Mwangesi alimtembelea Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Homera ofisini kwake ambapo katika mazungumzo yao walikubaliana kupitia Ofisi ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Kanda ya Nyanda za Juu Kusini iliyopo mkoani humo kuendelea kushirikiana katika kukuza uadilifu miongoni mwa viongozi wa umma katika mkoa huo.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Homera alimweleza Kamishna wa Maadili kuwa amelazimika kuitisha Semina ya Maadili kwa viongozi wote wa taasisi za serikali katika mkoa huo kwa sababu mkoa wa Mbeya una mambo mengi ikiwemo changamoto za kimaadili.

Kwa mujibu wa Mhe. Homera, mkoa huo unatekeleza miradi mingi ya serikali na wakati mwingine inaibuka migongano ya kimaslahi kwa baadhi ya viongozi wa umma wanaosimamia miradi hiyo bila ya wao wenyewe kujua hivyo ni matarajio yake kuwa elimu ya maadili itakapotolewa kwa viongozi hao itasaidia kuondoa migongano hiyo.

Mhe. Mwangesi yupo katika ziara ya siku mbili mkoani Mbeya ambapo kesho tarehe 23 Septemba, 2021 anatarajia kuzungumza pamoja na kutoa elimu kwa viongozi wote wa mkoa wa Mbeya pamoja na viongozi wa taasisi zote za serikali zilizopo mkoani humo.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >