JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Muongozo wa Uhakiki wahuishwa.
27 Oct, 2023
Muongozo wa Uhakiki wahuishwa.

Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa umma kuhuisha mwongozo wa uhakiki waRasilimali , Maslahi na Madeni ya Viongozi wa Umma katika kikao kazi kilichofanyika katika ukumbi wa Point Zone Jijin Arusha tarehe 30 Mei 2022.

Akifungua kikao kazi hicho Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji Sivangilwa Mwangesi alieleza kuwa ipo haja ya mwongozo wa uhakiki kuhuishwa kutokana na uhitaji uliosababishwa na maendeleo yaliyoletwa na matumizi mapana ya TEHAMA na tabia ya baadhi ya Viongozi kutokua waadilifu.

Mhe. Kamishna aliongeza kuwa Lengo la kuhuisha mwongozo huo sio tu kuwajengea uwezo wa uhakiki mali lakini kunawawezesha kuzingatia Maadili ya uhakiki, Sheria ,Kanuni na taratibu zenye kulinda heshima ya watumishi na Sekretarieti kwa ujumla.

“Kazi yoyote nzuri inategemea weledi wa watendaji hivyo basi ili kufanikisha hilo mwongozo wa uhakiki pia umeainisha maadili ya uhakiki na wahakiki wakati wa zoezi husika”alisema Mhe. Kamishna

Pamoja na hayo katika hotuba yake Mhe. Kamishna alifafanua kwamba kutokana na marekebisho katika Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma yaliyofanyika mwaka 2006 Sekretareti ya Maadili ilianza zoezi la uhakiki wa rasilimali na madeni ili kujiridhisha na uhalisia wa uhalali wa mali alizotamka kiongozi kama zinatokana na vyanzo vyake halali vya mapato. Pia kuhakikisha kama anashughulika na rasilimali na maslahi hayo bila kuleta mgongano wa maslahi.

Mhe. Kamishna aliendelea kufafanua kuwa lengo la msingi la uhakiki limekua ni pamoja na kuthibitisha kama Tamko la Rasilimali, Maslahi na Madeni linalotolewa na Kiongozi wa Umma ni sahihi; kujiridhisha kama thamani ya mali iliyotajwa katika tamko la Kiongozi inawiana au ndiyo thamani halisi ya mali husika.

Sambamba na hayo ni kutambua kama kuna rasilimali nyinginezo ambazo kwa makusudi hazikutamkwa; kutambua kama Kiongozi ana vyanzo Vingine vya mapato ambavyo hakuvitamka kwenye tamko lake na kutambua kama kuna rasilimali, maslahi au shughuli zinazo mwingiza Kiongozi kwenye Mgongano wa Maslahi.

Mhe. Kamishna alisisitiza kuwa Sheria inawataka Viongozi wa Umma kutekeleza majukumu yao kwa uaminifu, huruma ,umakini kujizuia na tamaa na kuridhika,kutoa tamko la Rasilimali , Maslahi na Madeni, kutopendelea, kujizuia na mazingira yatakayosababisha mgongano wa Maslahi, kutangaza hadharani maslahi ya fedha na kutoa Tamko la Kimaslahi kuhusu mikataba yao au na Serikali

Sekretarieti iliandaa mwongozo wa uhakiki ambao umekua ukiboreshwa kuendana na wakati. Mwongozo huu kwa mara ya mwisho ulirekebishwa mwaka 2021 ili kuongeza suala la uhakiki wa mgongano wa maslahi kutokana na kutungwa kwa Kanuni za Udhibiti wa Mgongano wa Maslahi za mwaka 2020.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >