JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Mkuu wa Mkoa wa Sindida awataka watumishi wa umma kuzingatia uadilifu wanapotekeleza majukumu yao.
11 Dec, 2024
Mkuu wa Mkoa wa Sindida awataka watumishi wa umma kuzingatia uadilifu wanapotekeleza majukumu yao.

Watumishi wa umma mkoani Singida wamewatakiwa kuzingatia  suala zima  la uadilifu  wanapotekeleza majukumu yao ikiwa ni pamoja na kutoa huduma kwa  kuzingatia haki kwa kila mmoja.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Bi. Halima Dendego ametoa wito huo katika  Kongamano la Maadhimisho  ya kilele cha Siku ya Maadili na Haki za Binadamu, lililofanyika  tarehe 10 Desemba,2024 katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa  wa Singida.

"Siku hii ina maana kubwa sana kwetu. Sisi watumishi wa umma tunatakiwa kujitafakari kwa namna tunavyotekeleza wajibu wetu katika kutoa huduma kwa umma kuwa tunatakiwa kufanya hivyo kwa kuzingatia haki za binadamu, kuwa waadilifu na kuepuka vitendo vya rushwa.’’alisema.

Kwa mujibu wa Mkuu huyo wa Mkoa, Kongamano hilo ni muhimu  kwa sababu linatoa  nafasi kwa viongozi na watumishi  wa umma kujitathmini na pia  kutathmini mchango wao katika kufikia lengo la Serikali la kikatiba la kuleta ustawi kwa wananchi wake.

Kongamano hilo lilijumuisha watumishi wa umma wa Sekretarieti ya Mkoa wa Singida, halmashauri ya Wilaya ya Sindida pamoja na taasisi nyingine za umma mkoani humo.

‘’Ni muhimu kutumia Kongamano hili kujitathmini na pia kufanya kazi kwa  kujielekeza kutoa huduma nzuri kwa wananchi, kuzingatia uadilifu wa hali ya juu na kutenda matendo mema yenye kuleta faraja kwa wananchi wetu,’’ alisisitiza Bi. Dendego.

Awali akitoa neno la utangulizi katika Kongamano hilo,  Katibu Msaidizi Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kati, Dodoma Bi. Jasmin Awadhi amesema kuwa Kongamano hilo linatokana na matukio mawili muhimu Duniani.

‘’Maadhimisho haya ni muunganiko wa matukio mawili ya Kimataifa. Kwanza ni Siku ya Mapambano dhidi ya Rushwa ambayo Mkataba wake ulisainiwa mjini Merida Mexico tarehe 9 Desemba, 2003 ambayo huitwa siku ya Maadili na siku ya pili ni Siku ya Haki za Binadamu iliyotokana na Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Binadamu uliosainiwa tarehe 10. 12.1948,” alisema.

Kwakuwa nchi yetu uadhimisha siku ya Uhuru tarehe 9 kila Desemba, Serikali iliamua kusongeza mbele Siku ya Maadili na kuiadhimisha tarehe 10 ambayo pia ni Siku ya Haki iza Binadamu. Tangu mwaka 2016, Serikali iliunganisha siku hizo mbili na kuziita Siku ya Maadili na Haki za Binadamu.

Kauli mbiu ya maadhimisho ya mwaka 2024 ilikuwa “Tumia haki yako ya kidemokrasia chagua Viongozi waadilifu na wanaozingatia haki za binadamu na misingi ya utawala bora kwa maendeleo ya Taifa.”

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >