JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

MKUU WA MKOA WA MARA AMEWATAKA VIONGOZI WA UMMA KUTOA MATAMKO YAO YA RASLIMALI NA MADENI KWA WAKATI.i
19 Dec, 2024
MKUU WA MKOA WA MARA  AMEWATAKA VIONGOZI WA UMMA KUTOA  MATAMKO YAO YA RASLIMALI NA MADENI  KWA  WAKATI.i

Mkuu wa Mkoa wa Mara  Kanali  Evans  Mtambi  ametoa wito kwa Viongozi wa Umma mkoani  humo n kutoa matamko yao ya Raslimali na Madeni kwa wakati hasa katika kipindi hiki tunapokaribia mwisho wa mwaka kwa lengo la kuweka  uwazi na kudhibiti matumizi mabaya  ya madaraka.

Kanali  Mtambi ametoa wito huo alipokuwa akifungua mafunzo kuhusu  Maadili ya Viongozi wa Umma yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi  ya Mkuu wa Mkoa mkoani  Mara  tarehe 17 Desemba 2024.

“Tuko  mwishoni mwa mwaka ambapo viongozi wote wa Umma wanapaswa kutoa kutoa matamko yao kwa mwaka 2024 ili kukidhi matakwa ya kisheria.”amesema.

Aidha Kanali  Mtambi katika hotuba yake alifafanua kuwa  mafunzo haya yataongeza nidhamu na ufanisi katika utekelezaji wa majukumu serikalini pia ni kielelezo cha dhamira ya Serikali ya awamu ya sita ya kuhakikisha kuwa suala la Maadili, Uadilifu na Uwajibikaji unaeleweka kwa wadau wote wa sekta ya Umma pamoja na sekta binafsi.

Ameongeza kuwa Maadili yana umuhimu mkubwa katika kujenga Imani ya Wananchi kwa viongozi wa Serikali kuhakikisha kuwa usimamizi wa Raslimali za Umma, kudhibiti mianya ya Rushwa, kuimarisha usimamizi wa sharia, kanuni na taratibu za utumishi wa umma na kudumisha Amani na utulivu na umoja wa kitaifa.

Kanali Mtambi alibainisha kuwa wapo viongozi wa Umma wasio waadilifu  wamekuwa wakijihusisha na vitendo vinavyopelekea uwepo wa mgongano wa Maslahi kati ya na Taasisi wanazozisimamia nna kwamba suala hili linapunguza kasi ya ukuaji wa uchumi na kurudisha nyuma juhudi za Serikali za utoaji huduma kwa jamii.

  Mafunzo hayo yaliwashirikisha Viongozi wa Umma wa Mkoa wa Mara wakiwemo wakuu wa Idara na Vitengo, Waheshimiwa Madiwani  ambapo  mada mbili zilijadiliwa ambazo ni Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma pamoja  Ujazaji wa Matamko ya Raslimali na Madeni kwa njia ya Mtandao.  (Online Decralation System-ODS).

 

 

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >