JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

MKURUGENZI TACAIDS AFIKISHWA MBELE YA BARAZA LA MAADILI KWA TUHUMA ZA MATUMIZI MABAYA YA MADARAKA
27 Oct, 2023
MKURUGENZI TACAIDS AFIKISHWA MBELE YA BARAZA LA MAADILI KWA TUHUMA ZA MATUMIZI MABAYA YA MADARAKA

Mkurugenzi Tathimini na Ufuatiliaji wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI nchini (TACAIDS) amefikishwa mbele ya Baraza la Maadili ya Viongozi wa Umma jijini Dodoma kwa makosa mawili likiwemo la matumizi mabaya ya matumizi ya madaraka na rasilimali za umma.

Dkt. Jerome Philip Kamwela anadaiwa kutenda kosa hilo tarehe 5/6/2019 majira ya saa 8 usiku maeneo ya Mbezi Beach katika halmashauri ya wilaya Kinondoni, Dar es Salaam.

Hata hivyo, taarifa za ajali hiyo zilitolewa na mlalamikiwa tarehe 23/9/2019 baada ya mwajili kupata malalamiko kutoka jeshi la polisi wilaya ya Kinondoni.

Wakili wa Serikali Fikiri Ngakonda alidai kuwa, “mnamo tarehe 5/6/2019 majira ya saa 8 usiku katika eneo la Mbezi Beach, Manispaa ya Kinondoni, Dar es Salaam mtuhumiwa alitumia gari ya ofisi yenye namba za usajili DFPA 2055 Toyota Land Cruser Prado kinyume na taratibu na kusababisha ajali kwa kugonga mnazi uliopo katika uzio wa nyumba ya Bi. Josephine Kombo na kuleta uharibifu wa gari na ukuta wa nyumba.”

Wakili Ngakonda ametaja kosa la pili kuwa ni kushindwa kutoa taarifa mahali popote kuhusu tukio hilo kinyume na taratibu za matumizi ya magari ya umma.

“Dkt. Kamwela baada ya kusababisha ajali bila sababu ya msingi hakutoa taarifa ya tukio hilo katika kituo chake cha kazi wala polisi kinyume na kifungu cha 6(1)(a) cha Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma,” amesema.

Wakili Ngakonda alidai mbele ya Baraza kuwa kitendo hicho ni kinyume na matakwa ya vifungu vya 12(1)(d) na 6(1)(a) vya Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma Na. 13 ya mwaka 1995, na hivyo kukiuka maadili ya viongozi wa umma kwa mujibu wa kifungu cha 6(2).

Imedaiwa mbele ya Baraza kuwa kibali cha gari hilo kinamtaka mtumiaji kutumia gari kwa matumizi ya umma ikiwemo kutoka nyumbani hadi kazini ama akitekeleza matujukumu ya umma wakati wa kazi ndani ya Dar es Salaam.

Hata hivyo, pamoja na mtuhumiwa kukana kosa, alikili kuwa alipata ajali kama Baraza lilivyoelezwa.

Dkt. Kamwela amelieleza Baraza kuwa, “Ni kweli nilipata ajali siku tajwa na nililifanyia gari matengenezo kama jambo la dhalula kwasababu yalikuwa madogo.”

Aliongeza kuwa, “dereva yeyote anaweza kupata ajali. Sikupata ajali kwasababu ya ukiukwaji wa maadili wala sikuwa na nia ovu.”

Alipoulizwa na Wakili wa Serikali kwanini hakutoa taarifa za tukio hilo kwa mwajili wake na katika jeshi la polisi kama taratibu zinavyoelekeza, Dkt. Kamwela alisema, “sikutoa taarifa mahali popote kwasababu madhara yalikuwa madogo.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >