JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Mkuchika azindua Maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za Binadamu.
27 Oct, 2023
Mkuchika azindua Maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za Binadamu.

Mkuchika azindua Maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki zaBinadamu.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Mkuchika (Mb) amezindua maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za Binadamu kitaifa Jijini Dodoma.

Katika Hotubayake Mhe. Waziri alisema kuwaSiku ya Maadili na Haki za Binadamu inayoadhimishwa hapa nchini kila mwakaimetokana na maadhimisho ya siku mbili tofauti ambazo huadhimishwa kitaifa ,yaani Siku ya Kimataifa ya Kupambana na Rushwa na Siku ya Kimataifa ya Haki za Binadamu.

Mhe.Waziri alieleza kuwa jukumu kubwa la Serikali ni kuwaletea wananchi maendeleo hivyo usimamizi wa maadili mema, haki za binadamu na mapambano dhidi ya rushwa linatakiwa kuwa suala endelevu kwa kuwa ndio msingi wa utoaji huduma inayokidhi matarajio ya Umma.

Mhe. Waziri aliendelea kusema kuwa ni dhahiri kwamba Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Mhe. Dkt John Pombe Mgufuli imefanya kazi kubwa katika kusimamia misingi ya maadili na utawala bora.

Kwa mujibu wa Mhe. Mkuchika juhudi hizo zinatambulika ndani na nje ya nchina kwa miaka ya hivi karibuni nchi yetu imekuwa inatolewa mfano wa nchi zilizofanikiwa sana katika masuala ya uadilifu, mapambano dhidi ya rushwa na matumizi mazuri ya rasilimali za nchi.

“utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uchumi umekuwa ukidumazwa kwa kiasi kikubwa na vitendo vya rushwa na ukiukwaji wa haki za binadamu ambako kunachangiwa na ukosefu wa maadili kwa baadhi ya watendaji katika nyanja zote”.

“Hivyo basi kwa kutambua ukubwa wa changamoto hiyo Serikaliya Awamu ya Tano imekuwa na mikakati mbalimbali inayoainishwa majukumu ya kila sekta ikiwa ni pamoja na Mkakati wa Taifa Dhidi ya Rushwa na Mpango wa Utekelezaji Awamu ya tatu ( National Anti-Corruption Strategy and Action Plan-NACSAP111) uliozinduliwaDesemba 2016”.Alifafanua Mhe. Mkuchika.

Mhe. Mkuchika aliongeza kusema kuwa unapozungumzia haki za binadamu huwezi kuepuka kuzungumzia huduma mbalimbali ambazo mwanadamu huzihitaji katika maisha yake ya kila siku ikiwa ni pamoja na huduma za afya na elimu ambapo upatikanaji wa huduma hizo hapa nchini umeboreshwa na unaendelea kuboreshwa ili kukidhi mahitaji na viwango.

Aidha Mhe. Waziri alimaliza kwa kutoa rai kwa waandishi wa habari kutafsiri na kuonyesha matokeo ya juhudi za Serikali katika kuimarisha Maadili, mapambano dhidi ya rushwa na uzingatiaji wa haki za binadamu.

Kwa mujibu wa Mhe. Mkuchika jambo hili ni muhimu sana wananchi kufahamu na kuifanya jamii nzima kuwa na maadili mema, kuheshimu haki za binadamu na kuchukia na kupiga vita rushwa ili kuiunga mkono azma ya Serikali katika kuimarisha maadili nchini.

Maadhimisho ya mwaka huu yatafanyika kwa kongamano litakalohusisha taasisi zisizo za kiserikali pamoja na wabia wa maendeleo na kauli mbiu itakua “Uzingatiaji wa Ahadi ya Uadilifu kwaViongozi na Watumishi kwa Ustawi wa Utawala Bora na Haki za Binadamu nchini”

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >