JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

MHE. DKT SAMIA SULUHU HASSAN AMWAPISHA JAJI (Mst.) TEEMBA KUWA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAADILI.
29 Aug, 2023
MHE. DKT SAMIA SULUHU HASSAN AMWAPISHA JAJI (Mst.) TEEMBA KUWA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAADILI.

Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amemwapisha Jaji (Mst.) Rose Teemba kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Maadili katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu Chamwino jijini Dodoma tarehe 23.5.2023.

Mhe. Rais alimteua Jaji Teemba tangu tarehe 24.4.2023 kwa mujibu wa kifungu cha 26(1) cha Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma Na. 13 ya 1995 kinachoeleza kuwa Baraza la Maadili litakuwa na wajumbe watatu watakaoteuliwa na Rais, miongoni mwao akiwemo aliyeteuliwa kutoka miongoni mwa watu wenye wadhifa au wamewahi kuwa na wadhifa wa Jaji wa Mahakama Kuu.

Aidha, kifungu hicho cha 26(3) kinasema kuwa Rais, atateua mmojawapo wa Wajumbe wa Baraza kuwa Mwenyekiti.

Katika hafla hiyo, Mhe. Rais ameeleza kuwa hana mashaka na uzoefu katika utendaji kazi waJaji Teemba.

“Jaji Sivangilwa Mwangesi, Kamishna wa Maadili akisha maliza kazi yake anakuleteeni nyinyi Baraza la maadili, ichambueni vizuri na kutuletea mapendekezo yenu,” amesema na kuongeza kuwa, “Tuna matatizo makubwa kwenyey eneo la uadilifu katika utawala, shughulikieni.”

Kazi kubwa ya Baraza la Maadili ni kufanya uchunguzi wa kina wa malalamiko yanayohusu ukiukwaji wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma dhidi ya viongozi wa umma waliotajwa katika kifungu cha 4 cha Sheria hiyo.

Aidha, uchunguzi huo hutanguliwa na uchunguzi wa awali ambao kwa mujibu wa kifungu cha 18(2)(c) cha Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma, hufanywa na Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma.

Jaji mstaafu Teemba anachukua nafasi ya Jaji mstaafu Ibrahim Mipawa aliyemaliza muda wake, akiongoza Baraza hilo tangu Agosti 16, 2019 alipoteuliwa kushika wadhifa huo.

Jaji mstaafu Teemba anakuwa Mwenyekiti wa tano wa Baraza la Maadili toka kuanzishwa kwake akitanguliwa na Jaji mstaafu Damian Lubuva, Jaji mstaafu Hamis Msumi, Jaji mstaafu Januari Msofe na Jaji mstaafu Ibrahim Mipawa.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >