JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

MADIWANI WA HALMASHAURI YA JIJI LA MWANZA WAMETAKIWA KUZINGATIA SHERIA YA MAADILI.
27 Oct, 2023
MADIWANI WA HALMASHAURI YA JIJI LA MWANZA WAMETAKIWA KUZINGATIA SHERIA YA MAADILI.

Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza, wametakiwa kuzingatia Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma ili kujiepusha na vitendo vinavyopelekea kuwepo kwa Mgongano wa Masilahi katika utekelezaji wa Majukumu yao ya kila siku.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu Msaidizi wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Ziwa Bwana Godson Kweka katika mafunzo ya Madiwani wa jiji hilo kuhusu Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma na 13 ya mwaka 1995, Kanuni za Serikali za Mitaa za mwaka 2000 na mgongano wa Maslahi.

Aidha Bw. Kweka aliwataka Madiwani hao kuzingatia Kiapo cha Ahadi ya Uadilifu walichoapa na wajibu wao katika kutekeleza kanuni za Serikali za Mitaa za mwaka 2000.

Akifungua mafunzo hayo Katibu Msaidizi anayeshughulikia Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza Bibi Christina Bigambo alisema mafunzo hayo yanategemewa kuwa chachu ya ushirikiano kati ya Madiwani wa Jiji la Mwanza pamoja na Watendaji wa Jiji kwa nia ya kuboresha utendaji na kuongeza ufanisi wa kazizao za kila siku.

Bibi Bigambo aliongeza kuwa Madiwani wanatakiwa kuzingatia Mada zote zitakazotolewa na Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ili ziwasaidie katika kuboresha utendaji wa kazi zao za kila siku kwa kufuata Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma.

Mafunzo hayo yalifungwa rasmi na Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Bibi Amina Makilagi ambapo aliwahimiza Madiwani hao kuzingatia mafunzo waliyoyapata katika kuwatumikia wananchi kwa weledi na uadilifu mkubwa.

Mafunzo hayo ya siku mbili yalihudhuriwa na Madiwani 26 wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza, ambapo yalifanyika katika ukumbi wa Halmashaurihiyo jijini Mwanza.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >