JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

MAAFISA WAANDAMIZI WA JESHI LA POLISI WAMETAKIWA KUZINGATIA MAADILI:
04 Dec, 2023
MAAFISA  WAANDAMIZI  WA  JESHI  LA  POLISI  WAMETAKIWA  KUZINGATIA  MAADILI:

MAAFISA  WAANDAMIZI  WA  JESHI  LA  POLISI  WAMETAKIWA  KUZINGATIA  MAADILI:

Maafisa  Waandamizi wa Jeshi  la Polisi Zanzibar wametakiwa kufanyakazi kwa Uadilifu na weledi mkubwa wnapotekeleza Majukumu yao kwa dhamana waliyopewa ili kujenga imani kwa wananchi wanaowaongoza pamoja na Serikali kwa ujumla.

Kauli hiyo imetolewa na Kamishna wa Polisi Zanzibar CP Hamad Khamis Hamad alipokuwa akifungua mafunzo ya Maadili kwa Maafisa  waandamizi wa Jeshi la Polisi yaliyofanyika katika Chuo cha Polisi Zanzibar tarehe 29 Novemba 2023.

Kamishna Hamad  katika  hotuba yake ameeleza kuwa, jamii ikikosa imani na jeshi la polisi  yaweza kupelekea  amani ya nchi kutoweka na kusababisha migogoro nchini.

Aidha Kamishna Hamad alibainisha  kuwa “kusimamia sharia bila uadilifu yaweza kusababisha machafuko katika nchi yetu” alisema.

Kamishana huyo pia alifafanua kuwa matendo yanayofanywa na jeshi la polisi katika kusimamia sharia ni lazima yawe ya mfano katika jamii na Serikali kwa ujmla.

Awali akimkaribisha mgeni rasmi, Katibu Msaidizi Kanda Maalumu Bi Eliza Komba amewataka Maafisa hao kuwa mstari wa mbele katika kusimamia Maadili katika kutekeleza Majukumu yao kwa Uadilifu na weledi wa kiwango cha juu.

Bi Komba pia amewataka Maafsa hao kuyaishi yote yatakayofundishwa katika mafunzo hayo kupitia Mada mada mbali mbali zilizoandaliwa katika utekelezaji wa kazi zao za kila siku.

Amefafanua kuwa miongoni mwa Mada zitakazojadiliwa ni pamoja na Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Mgongano wa Maslahi, Ahadi ya Uadilifu pamoja na Tamko la Raslimali na Madeni.

Mafunzo hayo yaliwashirikisha Maafisa Waandamizi wa jeshi la Polisi  kutoka Mikoa mitatu ya  Unguja. Mkoa wa Mjini, Kaskazini Unguja na Mkoa wa Kusini Unguja.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >