JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

MAAFISA WA JESHI LA POLISI WASISITIZWA KUZINGATIA KIAPO CHA UADILIFU.
20 Feb, 2024
MAAFISA WA JESHI LA POLISI WASISITIZWA KUZINGATIA KIAPO CHA UADILIFU.

Maafisa waandamizi wa Jeshi la Polisi nchini wametakiwa kuzingatia masharti ya kiapo cha Ahadi ya Uadilifu pamoja na sheria nyingine za nchi.

Wito huo umetolewa na Katibu Ukuzaji  Maadili, Bw. Waziri Kipacha mara baada ya kuongoza kiapo cha Ahadi ya Uadilifu kwa maafisa wandamizi 155 wa Jeshi la Polisi waliopandishwa vyeo mbalimbali na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. 

Hafla hiyo ilifanyika makao makuu ya Jeshi la Polisi jijini Dodoma, tarehe 19 Februari, 2024 na kuhudhuriwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Camillus Wambura.

Bw. Kipacha alieleza kuwa kiapo cha Ahadi ya Uadilifu kilianzishwa ili kuongeza nguvu kwenye sheria, kanuni na maadili yaliyopo.

"Nimesikia wimbo wa maadili kutoka Jeshi la Polisi ni wimbo ambao umegusa mambo mengi yaliyopo kwenye kiapo mlicho apa muda mfupi uliopita, hivyo mambo hayo mkiyazingatia yatawasaidia katika utendaji wenu wa kazi wa kila siku kwa kuzingatia maadili, sheria na  kanuni." Bw. Waziri Kipacha.

Bw. Kipacha aliwataka maafisa hao kutambua kuwa kiapo hicho ni dhamira ya ndani inayowaongoza kuwa waadilifu kwa kuzingatia misingi ya maadili na mikakati ya mapambano dhidi ya Rushwa.

"Sisi tunaimani na Jeshi la Polisi kuwa na nidhamu ya hali ya juu tunategemea maafisa mliokula kiapo cha Ahadi ya Uadilifu kuwa mfano kwa viongozi  wote kwa kuzingatia uadilifu," alisema

Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, Naibu Kamishna wa Polisi DCP, David Misime ambaye ni miongoni mwa maafisa waliokula kiapo cha Ahadi ya Uadilifu akiongea kwa niaba ya wenzake alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, kwa kufanikisha kuwapandisha vyeo maafisa hao na kumuhaidi kuwa vyeo hivyo vitawaongezea morali wa kazi na watavitumia kwa maendeleo ya Nchi na Jeshi la Polisi.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >