JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

PO-ETHICS SECRETARIAT Logo
Maafisa Ununuzi na Ugavi Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma wajengewa uwezo
27 Apr, 2026
Maafisa Ununuzi na Ugavi Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma wajengewa uwezo

Maafisa Ununuzi na Ugavi kutoka Ofisi ya Rais ,Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Makao Makuu na Kanda wamekutana  katika kikao kazi chenye lengo la kuwajengea uwezo katika kurekodi, kutunza na kusimamia mali za Taasisi.

Kikao kazi hicho kimefanyika tarehe 27 Aprili, 2026 katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT) mkoani Singida na kufunguliwa na Kamishna wa Maadili nchini Jaji (Stahiki) Sivangilwa Mwangesi.

Katika hotuba Jaji Mwangesi amewataka Maafisa hao kuhakikisha kuwa mifumo ya usimamizi wa mali inafanya kazi kwa ufanisi, kutoa ushauri unazingatia weledi na kuisaidia Taasisi kuepuka hasara kwa kuboresha matumizi ya rasilimali.

“Jukumu lenu halipo tu katika kutekeleza taratibu bali linaenda mbali zaidi hadi katika kutoa ushauri sahihi wa kitaalamu na unaozingatia sheria na kanuni katika usimamizi wa mali za umma,” alisema Mhe. Mwangesi.

Aidha Jaji Mwangesi ameongeza kuwa ni muhimu kwa Maafisa Ununuzi na Ugavi kuhakikisha kuwa wanatoa taarifa sahihi ambazo ni muhimu katika muktadha wa ukaguzi kwani Taasisi nyingi utathiminiwa kupitia ukaguzi unaofanywa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

“Moja ya matarajio ya Taasisi ni kupata hati safi na itambulike kuwa hati safi haipatikani kwa bahati mbaya bali inatokana na mifumo imara, nidhamu ya kazi na zaidi ya yote ni uwepo wa taarifa sahihi na zinazoaminika,” alisisitiza.

Kiongozi huyo ameongeza kuwa iwapo taarifa zilizomo katika daftari la mali la Taasisi hazilingani na hali halisi au hazijakamilika na kuhuishwa kwa wakati uwezekano wa kupata hoja za ukaguzi huwa mkubwa na hoja hizo huathiri taswira ya Taasisi, huathiri utendaji wake pamoja na uaminifu mbele ya wadau wake.

Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Usimamizi na Manunuzi Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Bw. Kenedy Mwakalindile amesema kuwa kikao kazi hicho cha siku tatu kimelenga katika kutoa mafunzo na kuboresha utendaji kazi na kuhakikisha kuwa wanakua na daftari lenye taarifa sahihi.

“Lengo la kukutana hapa ni kupitia daftari letu kwa pamoja na pia kulifanyia maboresho ili tuwe na daftari sahihi ambalo litatusaidia hapo mbeleni hasa kwenye ukaguzi kutoka nje,” alisema Bw. Mwakalindile.

Katika kikao kazi hicho mada mbalimbali zimetolewa ikiwemo namna ya matumizi ya Mfumo wa Kieletroniki wa Usimamizi wa Mali za Serikali (GAMIS).

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >