MAAFISA TEHAMA WATAKIWA KUWA MABALOZI KATIKA KUWAELEKEZA VIONGOZI MATUMIZI YA MFUMO WA ODS.
Wakuu wa Vitengo vya TEHAMA nchini wametakiwa kuwa mabalozi wazuri katika kuwaelekeza viongozi katika maeneo yao kuhusu matumizi ya mfumo wa ODS- (On Line Declaration System) ili kuwasaidia viongozi kujaza Matamko yao kwa njia ya mtandao kwa urahisi, umakini na kwa usahihi zaidi.
Kauli hiyo imetolewa na Katibu Msaidizi Kanda ya Kaskazini Arusha Bw. Gelard Mwaitebele alipokuwa akifungua mafunzo ya Maadili kwa baadhi ya Wakuu wa Vitengo vya TEHAMA kutoka katika mikoa ya Arusha, Manyara na Kirimanjaro yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Arusha tarehe 12 Februari 2026.
Bw. Mwaitebele katika hotuba yake amefafanua kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uelewa wa pamoja na wa kina kuhusu matumizi ya mfumo wa ODS ili kuwasaidia viongozi walioko katika maeneo yao ya kazi kujaza Matamko yao kwa njia ya mtandao kwa weledi, usahihi na kwa umakini zaidi kwa manufaa yao na Taifa kwa ujumla,
Aidha, Bw. Mwaitebele katika hotuba yake amezitaja baadhi ya faida za matumizi ya mfumo huo kuwa ni pamoja na kuongeza uwazi na uwajibikaji katika utumishi wa Umma kwa kuwawezesha viongozi kuwasilisha Matamko yao kwa wakati na kwa haraka kwa kujaza mali zao pamoja na mali za wenza wao na mali za watoto wao walio chini ya umri wa miaka 18 ambao awajaoa wala kuolewa.
Ametaja faida nyingine ya matumizi ya mfumo wa ODS kuwa ni pamoja na kupunguza gharama na muda uliokuwa ukitumika katika ujazaji na uwasilishaji wa fomu kwa njia ya kawaida na kupunguza matumizi ya karatasi ngumu kama ilivyokuwa hapo awali pamoja na kuimarisha usalama na uhifadhi wa taarifa za viongozi kwa umakini mkubwa.
Bw. Mwaitebele ameongeza kuwa faida nyingine ya matumizi ya mfumo huu ni kurahisisha ufuatiliaji na tathimini pamoja na kuharakisha mchakato wa uhakiki na uchambuzi wa matamko na kuongeza ufanisi wa utendaji wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa ujumla wake.
“Ni muhimu kutambua kuwa, mafanikio ya mfumo huu yanategemea ushiriano wenu nyinyi wataalamu wa TEHAMA katika Taasisi zenu hivyo mnayo dhamana ya kuhakikisha kuwa miundo mbinu ya teknolojia ipo sawa, changamoto za kiufundi zinatatuliwa kwa wakati na viongozi wanapatiwa mwongozo sahihi ambao mtaupata kupitia mafunzo haya”amesema.
Mafunzo haya yamewashirikisha Wakuu wa vitengo vya TEHAMA kutoka katika Halmashauri, Jiji, Miji kutoka katika mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, na Manyara.
Wakuu wa Vitengo vya TEHAMA nchini wametakiwa kuwa mabalozi wazuri katika kuwaelekeza viongozi katika maeneo yao kuhusu matumizi ya mfumo wa ODS- (On Line Declaration System) ili kuwasaidia viongozi kujaza Matamko yao kwa njia ya mtandao kwa urahisi, umakini na kwa usahihi zaidi.
Kauli hiyo imetolewa na Katibu Msaidizi Kanda ya Kaskazini Arusha Bw. Gelard Mwaitebele alipokuwa akifungua mafunzo ya Maadili kwa baadhi ya Wakuu wa Vitengo vya TEHAMA kutoka katika mikoa ya Arusha, Manyara na Kirimanjaro yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Arusha tarehe 12 Februari 2026.
Bw. Mwaitebele katika hotuba yake amefafanua kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uelewa wa pamoja na wa kina kuhusu matumizi ya mfumo wa ODS ili kuwasaidia viongozi walioko katika maeneo yao ya kazi kujaza Matamko yao kwa njia ya mtandao kwa weledi, usahihi na kwa umakini zaidi kwa manufaa yao na Taifa kwa ujumla,
Aidha, Bw. Mwaitebele katika hotuba yake amezitaja baadhi ya faida za matumizi ya mfumo huo kuwa ni pamoja na kuongeza uwazi na uwajibikaji katika utumishi wa Umma kwa kuwawezesha viongozi kuwasilisha Matamko yao kwa wakati na kwa haraka kwa kujaza mali zao pamoja na mali za wenza wao na mali za watoto wao walio chini ya umri wa miaka 18 ambao awajaoa wala kuolewa.
Ametaja faida nyingine ya matumizi ya mfumo wa ODS kuwa ni pamoja na kupunguza gharama na muda uliokuwa ukitumika katika ujazaji na uwasilishaji wa fomu kwa njia ya kawaida na kupunguza matumizi ya karatasi ngumu kama ilivyokuwa hapo awali pamoja na kuimarisha usalama na uhifadhi wa taarifa za viongozi kwa umakini mkubwa.
Bw. Mwaitebele ameongeza kuwa faida nyingine ya matumizi ya mfumo huu ni kurahisisha ufuatiliaji na tathimini pamoja na kuharakisha mchakato wa uhakiki na uchambuzi wa matamko na kuongeza ufanisi wa utendaji wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa ujumla wake.
“Ni muhimu kutambua kuwa, mafanikio ya mfumo huu yanategemea ushiriano wenu nyinyi wataalamu wa TEHAMA katika Taasisi zenu hivyo mnayo dhamana ya kuhakikisha kuwa miundo mbinu ya teknolojia ipo sawa, changamoto za kiufundi zinatatuliwa kwa wakati na viongozi wanapatiwa mwongozo sahihi ambao mtaupata kupitia mafunzo haya”amesema.
Mafunzo haya yamewashirikisha Wakuu wa vitengo vya TEHAMA kutoka katika Halmashauri, Jiji, Miji kutoka katika mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, na Manyara.v
