JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Maadhimisho ya siku ya Maadili na Haki za Binadamu yazinduliwa
03 Dec, 2023
Maadhimisho ya siku ya Maadili na Haki za Binadamu yazinduliwa

Maadhimisho ya siku ya Maadili na haki za binadamu yalizinduliwa rasmi tarehe   03 Desemba, 2023 katika hafla iliyofanyika katika Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma. Kauli mbiu ya maadhimisho hayo ni “Zingatia Maadili, Utu, Uhuru, na Haki kwa watu wote kwa maendeleo endelevu”

Akizindua maadhimisho hayo Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana alisema kuwa maadhimisho hayo yana lengo la kuwakumbusha viongozi, watumishi na wananchi kwa ujumla wake juu ya dhana nzima ya kuwa na  maadili, kukwepa vitendo vya rushwa, kuzingatia haki za binadamu, kufuata taratibu na kanuni mbalimbali za nchi jambo ambalo litaileta maendeleo katika jamii na Serikali kwa ujumla.

Mhe. Pindi aliendelea kusema kuwa jukumu la Serikali ni kuhakikisha kuwa inawaletea wananchi maendeleo hivyo usimamizi wa Maadili na mapambano dhidi ya rushwa na masuala ambayo lazima yatiliwe mkazo ili kuwa na viongozi, watumishi na jamii yenye madili na itakayokua mstari wa mbele katika kukwepa vitendo vya rushwa jambo ambalo litasaidia usimamizi na matumizi mazuri ya rasilimali za nchi.

“Serikali yetu chini ya Rais wetu mpendwa Mhe. Samia Suluhu Hassan imekua ikipeleka fedha nyingi katika miradi mbalimbali lakini fedha hizo zimekua zikiishia katika mifuko ya watu wachache waliokosa maadili na kukwamisha juhudi za Serikali yetu, niwaase ndugu zangu tushiriki kwa pamoja kusimamia maadili na kupinga vitendo vya rushwa na tuiunge Serikali yetu mkono ili sote tufurahie rasilimali za nchi yetu” alisema.

Pamoja na hayo  Mhe. Pindi alisema kuwa maadhimiso ya siku ya maadili na haki za binadamu yanapaswa kuwa endelevu ”Kuadhimisha siku hii kunatupa fursa ya kujitathmini ni wapi tulipotoka ni wapi tulipo na ni wapi tunaelekea katika suala zima la Maadili” alisema.

Katika hatua nyingine Mhe. Pindi alitumia fursa hiyo kuwaasa baadhi ya watendaji wa serikali wasiofuata taratibu katika kutoa haki badala yake wanadai rushwa kwa njia mbalimbali jambo ambalo ni utomvu wa maadili “wapo baadhi ya watendaji wenzangu wanaotumia vyeo na madaraka  yao vibaya kwa kudai rushwa kwa njia mbalimbali na kukiuka haki za binadamu kwa kutokutoa maamuzi ya haki, tunapaswa kujitafakari na kuzingatia viapo vyetu” alisema.

Shuhuli mbalimbali zitafanyika katika kuadhimisha Siku ya Maadili na Haki za Binadamu kwa mwaka 2023 ikiwa ni pamoja na kutoa elimu kwa umaa kupitia vyombo mbalimbali vya habari nchini, jukwaa la wadau wa masuala ya rushwa, wiki ya kutoa huduma kwa jamii pamoja na kilele cha maadhimisho hayo tarehe 10 Desemba,2023.

Maadhimisho ya siku ya Maadili na haki za binadamu nchini, imetokana na siku mbili tofauti ambazo huadhimishwa kimataifa ambazo ni Siku ya Kimataifa ya Kupambana na Rushwa pamoja na Siku ya Kimataifa ya Haki za Binadamu ambapo kuanzia mwaka 2016 Serikali iliamua kuadhimisha siku hizi kwa pamoja hivyo mwaka huu ni wa saba (7) kwa maadhimisho haya kufanyika kwa pamoja.

 

Maadhimisho hayo huratibiwa na taasisi zinazosimamia utawala bora ikiwa ni pamoja na  Ofisi ya Rais Ikulu, Ofisi ya Rais, Menejiment ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Sekretarieti ya Maadili ya  Viongozi wa Umma, Wizara ya Katiba na Sheria, Taasisi ya Kuzuia na kupambana na Rushwa, Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi, Tume ya Utumishi wa Umma, Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi, Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Serikali pamoja na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >