JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

KLABU MPYA 15 ZA MAADILI ZAANZISHWA WILAYANI MPWAPWA
29 Apr, 2025
KLABU MPYA 15 ZA MAADILI ZAANZISHWA WILAYANI MPWAPWA

Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kati, Dodoma imeanzisha klabu mpya 15 za Maadili kwa shule za msingi na sekondari katika Halmashauri ya  Wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma.

Klabu hizo, zilizinduliwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wlaya ya Mpwapwa Bi. Mwanahamisi Ally kati ya tarehe 22 hadi 25 Aprili, 2025 wakati wa zoezi maalum lililohusisha shule za msingi na sekondari zilizopo wilayani humo.

Bi. Mwanahamisi ameipongeza Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa jitihada  wanazofanya za kutoa elimu ya maadili kwa kada mbalimbali nchini.

‘’Kwa kweli niwapongeze katika hili maana mnafanya jambo ambalo lina manufaa makubwa kwa kizazi cha sasa na baadae kwa kutoa elimu ya maadili ambayo ni msingi kwa vijana hawa pamoja na Taifa zima,’’ alisema Bi. Mwanahamisi.

Shule za msingi zilizofanya uzinduzi wa klabu mpya ni; Tambi, Nana, Mwenzele, Mbori, Ikulu, Mlembule, Mpeta, Bumila, Kimaghai,Mapala, Manghangu na Vinghane, wakati shule za sekondari ni Mlembule, Kimaghai A na Kimaghai.

Akizungumza mara baada ya kufunguliwa kwa klabu ya Maadili shuleni kwake, Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Mlembule Bw. Stephano Mushi alishukuru Sekretarieti ya Maadili na uongozi wa Wilaya ya Mpwapwa kwa kuona umuhimu wa kuwa na klabu za Maadili na aliahidi kuisimamia vyema kwa kushirikiana na mwalimu mlezi.

‘’Tunashukuru kwa jambo hili, hii ni hatua kubwa kwetu na kutokana na changamoto za kimaadili zilizopo katika shule yetu, kuanzishwa kwa klabu kutawasaidia wanafunzi kujitambua na kuwa waadilifu na chachu katika kuleta mafanikio ya kitaaluma,’’alisema Mwalimu Mushi.

Kwa upande wake Afisa Maadili kutoka Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Bw. Joshua Mwambande alisema kuwa zoezi hilo ni endelevu kwa Kanda ya Kati yenye mikoa ya Dodoma na Singida na alisisitiza kuwa licha ya kufanikisha kuanzishwa kwa klabu hizo, Taasisi itafanya ziara za mara kwa mara kuangalia maendeleo ya klabu.

‘’Zoezi hili ni endelevu, tunaendelea kuanzisha klabu mpya na kuzihuisha klabu za zamani, tutazitembelea mara kwa mara kujua zipo katika hali gani,’’ alisisitiza Bw. Mwambande.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >