JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Jaji Mwangesi: Viongozi zingatieni Uadilifu
27 Oct, 2023
Jaji Mwangesi: Viongozi zingatieni Uadilifu

Jaji Mwangesi: Viongozi zingatieni Uadilifu

Viongozi wa Umma wametakiwa kuwa waadilifu katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku ili waweze kuaminika na kukubalika katika jamii inayowazunguka.

Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji wa Rufani Sivangilwa Mwangesi ametoa wito huo Juni 14, 2021 jijini Arusha wakati akitoa mada kuhusu maadili kwa viongozi wa umma katika kikao cha Viongozi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Arusha.

Mhe. Mwangesi alisema kuwa, “Ni ukweli usiopingika kwamba viongozi waadilifu wanakubalika katika jamii na ni chachu kwa wananchi kuiga mifano ya uadilifu kutoka kwa viongozi wao.”

Kwa mujibu wa Jaji Mwangesi, kiongozi wa umma anapaswa kujipambanua kwa watu anaowaongoza kwa kutimiza wajibu wake bila kushurutishwa na kutumia uwezo na ushawishi alio nao kujenga uadilifu katika jamii.

Aidha Kamishna alisisitiza kuwa, kiongozi yeyote wa umma anapaswa kuwa na tabia na mwenendo usio kuwa na mashaka ili wananchi wamwamini na kuiamini Serikali anayoitumikia.

Katika hatua nyingine Jaji Mwangesi aliwakumbusha viongozi kuzingatia misingi ya Maadili ya Viongozi wa Umma inayomtaka kila Kiongozi kuzingatia Maadili katika utekelezaji wa majukumu yake, Kuepuka mwenendo unaohaibisha utumishi wa umma baada ya kuacha wadhifa husika; hususani kujiepusha na tabia za ulevi, uhuni, kujihusisha na biashara zisizohalali.

“Katika kuzingatia misingi hiyo viongozi wanalazimika kuzingatia sheria, kanuni, taratibu pamoja na miongozo katika kutekeleza majukumu yao,”alisema.

Misingi ya maadili inayotakiwa kuzingatiwa ni pamoja na kufanya kazi kwa uaminifu, huruma, umakini, kujizuia na tamaa na kuzingatia viwango vya juu vya maadili kadri iwezekanavyo. Misingi mingine ni kuzingatia haki, kutopendelea na kutenda kazi kwa uadilifu wa hali ya juu ili kulinda na kuimarisha imani ya wananchi na serikali.

“Jiepusheni na migongano ya kimaslahi kwani hairuhusiwi kufanya jambo au kutoa uamuzi kwa kuzingatia maslahi binafsi. Epukeni kuzingatia maslahi ya familia zenu au mtu mwingine yeyote mliye na uhusiano naye,” alisisitiza.

Awali akifungua kikaohicho, Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. John Mongela alisema kuwa ipo changamoto kwa baadhi ya Viongozi wa Umma kudhani kuwa maadili yanahusika na ujazaji wa fomu za Tamko la Rasilimali na madeni tu.

Mhe. Mongela alifafanua kuwa Viongozi wengi wanatimiza tu kipengele cha Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma kinachowataka kakujaza Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni kila ifikapo mwisho wa mwaka, lakini mienendo yao sio mizuri na hairidhishi kwani baadhi ya viongozi ni walevi, watoro, watumiaji wa lugha isiyofaa, wezi wa mali za umma na tabia nyingine nyingi zinazoipa taswira mbaya dhana ya uongozi.

“Viongozi wa Umma tunatakiwa kuwa na madili mazuri yasiyotiliwa shaka na kuyaishi yale tunayopaswa kuzingatia kwani kiongozi yeyote katika ngazi au wadhifa wowote ni kioo cha jamii husika,” alisema.

Kikao hicho cha Kamishna wa Maadili na Viongozi wa Umma ni sehemu ya Maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma mwaka 2021 ambapo Mhe. Mwangesi anatembelea wadau wa maadili, kutoa elimu na kusikiliza kero na malalamikoo yao kwa lengo la kuboresha huduma zinazotolewa na Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >