JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

ELIMU YA UJAZAJI TAMKO LA RASLIMALI NA MADENI KWA MTANDAO YATOLEWA RUVUMA.
17 Dec, 2024
ELIMU YA UJAZAJI TAMKO LA RASLIMALI NA MADENI KWA MTANDAO YATOLEWA RUVUMA.

 

Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma imetoa mafunzo ya ujazaji na urejeshwaji wa Tamko la Raslimali na Madeni kwa njia ya Mtandao (Online Declaration System-DS) kwa Viongozi wa Umma wa mkoani Ruvuma pamoja na kuwakumbusha uzingatiaji wa masuala ya kimaadili wakati wanapotekeleza majukumu yao.

Mafunzo hayo yalifanyika ukumbi wa Bomba mbili tarehe 17 Desemba, 2024 mjini Songea na Viongozi wa Umma walioshiriki ni kutoka Kamati ya Usalama ya Mkoa na Wilaya, wakuu wa Taasisi zilizopo Ruvuma, Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri za Mkoa wa Ruvuma.

Akifungua mafunzo hayo, mgeni rasmi Katibu tawala Msaidizi (UTAWALA) Mkoa wa Ruvuma, Bw. Joel Mbewa aliwataka Viongozi wa Umma kujitahidi kuendana na mabadiliko ya kiteknolojia yanayolenga kuboresha utendaji kazi, kwani kwa sasa Serikali kila kitu kinakwenda kidigitali.

“Tumieni fursa hii kujifunza kwa bidii ili mfahamu vyema namna ya kutumia mfumo wa ODS kwani kama mnavyofahamu kuwa tarehe 31 ya mwezi Desemba ya kila mwaka, Viongozi wote tunatakiwa tuwe tumewasilisha Tamko la Rasilimali na Mdeni kwa Kamishna wa Maadili bila kuchelewa,” alisema Bw. Mbewa.

Katibu Msaidizi Idara ya Ukuzaji wa Maadili, Bw. Salvatory Kilasara alisema lengo la mafunzo haya ni kuwajengea uwezo Viongozi wa Umma namna ya kuwasilisha Tamko la Rasilimali na Madeni kwa njia ya Mtandao kwani kwa sasa haipokei tena Tamko kutoka kwa kiongozi kwa njia ya nakala ngumu.  

“kutokana na maendeleo ya Teknolojia Serikali kupitia Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa umma, imeturahisishia kazi ya kuwasilisha matamko hayo kwa kutumia mfumo wa ODS. Ni matumaini yangu kwamba kupitia mafunzo haya, kila mmoja wetu atanufaika na elimu hii ya ujazaji wa matamko haya kwa njia ya mtandao,” alisema Bw. Kilasara.

Kwa upande wake Katibu Msaidizi Sekretarieti ya Maadili Kanda ya Kusini, Bw. Filotheus Manula amewaambia Viongozi wa Umma kuwa Maadili kwa kiongozi wa Umma hayapimwi kwa kiongozi kuwa masikini au tajiri, kwani kiongozi anaweza kuwa masikini na akawa hana Maadili na kiongozi anaweza kuwa tajiri na akawa na Maadili.

Kiongozi wa umma ambaye atakuwa ametumikia utumishi wa Umma kwa zaidi ya miaka 10 lakini anakosa hata kumiliki kiwanja au nyumba au hana maendeleo yeyote, uyo kwetu tunamuona kama hana Maadili. Kwani Serikali inamlipa mshahara mzuri, anapata posho mbalimbali sasa anazipeleka wapi? Kwetu sisi hayo sio Maadili kwa Kiongozi wa Umma kwani tunahitaji Kiongozi wa Umma anayeleta maendeleo kwa wananchi na ya kwake Binafsi, alisema, Bw. Manula.

Afisa TEHAMA kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Bi Ester Allamani amewatoa hofu viongozi kuhusu matumizi ya mfumo kuwa ni mfumo rahisi ambao kila Kiongozi anaweza kutumia bila changamoto yeyote kama akifuata taratibu na maelezo ya mfumo.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >