JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Daftari la Vihatarishi la Sekretarieti ya Maadili kuhuishwa.
27 Oct, 2023
Daftari la Vihatarishi la Sekretarieti ya Maadili kuhuishwa.

Daftari la Vihatarishi la Sekretarieti ya Maadili kuhuishwa.

Baadhi ya watumishi wa Sekretarieti ya Maadili ambao ni Vinara wa Vihatarisi “Risk Champions” kutokamakao Makuu na Kanda kuhuisha daftari la vihatarishi la Taasisi la mwaka 2021/2022. Zoezi hilo limefanyika katika kikao kazi cha watumishi hao kilichofanyika Mjini Morogoro mapema wiki hii.

Akifungua kikao kazi kazi hicho Kamishna wa MaadiliMhe. JajiSivangilwa Mwangesi alisema kuwa kikao kazi hicho kina lengo la kuhuishadaftari hilo ikiwa ni utekelezaji wa maelekezo ya Mwongozo kutoka Wizara ya Fedha na mipango chini ya Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Serikali, ambapo inatakiwa kila Taasisi za Umma kuhuisha madaftari ya vihatarishi.

Mhe. Mwangesi alisema kuwa Ili kuhakikisha Sekretarieti ya Maadili inafanya kazi zake ipasavyo kwa ufanisi lazima Taasisi ifuate Sheria,Taratibu na miongozo inayotolewa katika kutekeleza majukumu yake.”hatuna budi kufanya kazi hii ya kuhuisha daftari la vihatarishi kwani ni agizo kutoka juu nasi tupo kwa ajili ya utekelezaji”

Aidha Mhe. Mwangesi aliwaasa watumishikufanya kazi kwa kujituma, kufuata sheria, Kanuni na taratibu ili kuifanya Sekretarieti ya Maadili iweze kusaidia Serikali katika kutimiza malengo yake.”Nasisitiza kuhakiksha mnaelewa na kuvifanyia kazi vipengele vinavyohusiana na masuala ya vihatarishi kwa ujumla wake ili muweze kutekeleza kwa ufanisi kazi hii”alisisitiza Mhe. Mwangesi.

Mhe. Mwangesi aliongeza kuwa ni jukumu la kila mmojakatika kazi hii kushiriki ipasavyo na kuzingatia yale yote yatakayowasilishwa na mwezeshaji ili sote tuwe na uelewa wa vihatarishi vya Taasisi.

Aidha kikao kazi hicho mbali na kuhuisha daftari la Taasisi lamwaka2021/22 wajumbe walipata wasaa wa kupitia na kuchambua namna nzuri na bora ya uandaaji wa Uchambuzi wa vihatarishi, mpango wa kudhibiti vihatarishi namwongozo wa kudhibiti vihatarishi katika Taasisi.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >