JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Uwasilishaji wa Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni
13 Dec, 2023

Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma inapenda kuwakumbusha viongozi wote wa umma walioainishwa kwa mujibu wa kifungu cha 4 cha Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma (Sura ya 398), kuwa upokeaji wa Tamko la Rasilimali, Maslahi  na Madeni kwa mwaka 2023, umeanza tangu tarehe 01 Oktoba, 2023 na utamalizika tarehe 31 Desemba, 2023.

Uwasilishaji wa Tamko hilo kwa Kamishna wa Maadili ni kwa mujibu wa kifungu cha 9(1)(b) cha Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma na kwamba kutoa Tamko la uongo, potofu, kuchelewa ama kushindwa kuwasilisha Tamko hilo kwa kipindi kilichoainishwa ni ukiukwaji wa maadili kwa mujibu wa kifungu cha 16 cha Sheria tajwa.

Kiongozi anatakiwa kupakua fomu katika tovuti ya Taasisi yenye anwani www.maadili.go.tz na kuijaza kisha kuwasilisha Tamko husika kwa kufika moja kwa moja katika Ofisi za Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Makao Makuu zilizoko Jengo la PSSSF Kambarage, Mtaa wa Jakaya Kikwete - Dodoma, Ofisi za Kanda ya Kati zilizoko Viwanja vya Nanenane – Dodoma, Ofisi za Kanda Maalum Dar es Salaam zilizoko Barabara ya Ohio karibu na Benki ya CRDB Holland House,  Dar es Salaam, Ofisi za Kanda ya Kaskazini zilizoko katika Jengo la Hazina – Arusha, Ofisi za Kanda ya Ziwa zilizoko Jengo la NSSF, Mtaa wa Kenyatta - Mwanza, Ofisi za Kanda ya Nyanda za Juu Kusini zilizoko Jengo la NHIF – Mbeya, Ofisi za Kanda ya Mashariki zilizoko Jengo la NSSF – Morogoro, Ofisi za Kanda ya Magharibi zilizoko Mkabala na Hoteli ya Orion – Tabora na Ofisi za Kanda ya Kusini zilizoko Jengo la Maadili – Mtwara, Mtaa wa Chikongola Barabara ya TANU. Aidha, kiongozi anaweza pia kuwasilisha Tamko kwa njia ya posta kupitia “registered mail” ikiwemo “ems.”  

Viongozi wanakumbushwa kuwa Tamko linalopokelewa ni nakala halisi (Original Copy) na sio lililorudufiwa (Photocopy) au lililokuwa “scanned” na kutumwa kwa njia ya baruapepe.

 

 

 

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >